Monday, May 5, 2014

SERIKALI MBILI ZATOSHA WAZANZIBAR WASEMA


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Zanzibar na kuwaambia CCM itasimamia haki za Wazanzibar na kuhakikisha Muungano unadumu na Mapinduzi ya Zanzibar yanaenziwa .

 Wananchi wakionyesha ishara ya Serikali mbili kwenye mkutano wa CCM kwenye viwanja vya Kibanda Maiti, Unguja Zanzibar.

 Kila mtu alionyesha mapenzi yake kwa CCM.


Wakazi wa Zanzibar hawakujali mvua iliyokuwa inanyesha kwenye mkutano wa CCM Kibanda Maiti Zanzibar

Mama Fatma Karume akihutubia wakazi wa Unguja na kuwaambia kuwa waasisi wetu waliweka uzio wa kutulinda na kudumisha umoja na undugu wetu na kusema uzio huo ni Muungano wetu.

Mbunge wa Songea Mjini Dk Emmanuel Nchimbi akihutubia wakazi wa Unguja kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kibanda Maiti na kuwataka wananchi hao kuwa makini na viongozi wanaogeuza maneno huku akitolea mfano kutoka kwenye kitabu cha Maalim Seif.

Sehemu ya Umati uliohudhuria mkutano wa hadhara ambao ulihutubiwa na Viongozi mbali mbali wa CCM wakiongozwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana. (FS)

source: mjengwa blog

No comments:

Post a Comment