Thursday, July 4, 2013

TUJIKUMBUSHE MATUKIO MBALIMBALI ZIARA YA OBAMA TANZANIA

     Rais Barack Obama alivyowasili Tanzania

 Maofisa Usalama wa Marekani, wakiingia Uwanja wa Ndgege wa Zamani, jijini Dar es Salaam, ilikotua ndege ya Rais Barrack Obama wa Marekani  kwa ajili ya kuimarisha ulinzi uwanjani hapo jana.


Rais wa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, Spika wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho, ni miongoni mwa Viongozi waliofika kumpokea Rais wa Marekani Barack Obama, alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Tanzania. 
Ndege iliomchukuwa Rais Obama ikiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere

Ndege ya Rais wa Marekani, Barrack Obama, 'Airforce One' ikiwa imetua tayari, uwajani hapo.
 
 
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete na Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Balozi Alfonso, wakiende kumpokea Mgeni wao Rais wa Marekani Barack Obama akiwasili katika Uwanja wa Mwalim  Nyerere kwa ziara ya Siku mbili kutembelea Tanzania akitokea Nchini Afrika ya Kusini. 
Rais wa Marekani akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalim Nyerere kwa ziara ya siku mbili, akiongozana na Mkewe na Watoto wake wakishuka katika ndege yake.  
Rais Obama akiteta na Mwenyeji wake Rais Kikwete alipowasili Tanzania akiwa katika ziara ya siku mbili Tanzania.
Rais Obama akiwa na Mwenyeji wake Rais wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete wakielekea katika jukwaa maalum aliloandaliwa kwa ajili ya kupingwa wimbo wa Mataifa haya mawili  
Rais wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akifurahia jambo na Rais wa Marekani Barack Obama. wakiwa katika uwanja wa ndege.

 

8E9U8352

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akisalimiana na Rais wa Marekani Barack Obama wakati alipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar leo
8E9U8357
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Kikwete akimtambulisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein kwa Rais wa Marekani Barack Obama
8E9U8374
Makamu wa pili wa Rais , Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Rais wa Marekani Barack Obama wakati alipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar leo
8E9U8382
Spika wa Baraza la wawakilishi , Zanzibar Pandu Ameir Kificho akisalimiana na Rais wa Marekani Barack Obama wakati alipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar leo

 

 
 










Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akizungumza na Rais wa Marekani Barack Obama, katika Ukumbi wa Ikulu Jijini Dar es Salaam jana, akiwa nchini katika  ziara ya siku mbili kwa mualiko wa kiserikali.

 alipowasili Uwanjani hapo kwa ajili ya kumpokea mgeni wake, Rais wa Marekani, Barrack Obama.


 

Rais Barraka Obama akishuka na mtoto wake mkubwa Mallya, uwanjani hapo, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza ziara yake ya siku mbili nchini.


Mke wa Rais wa Marekani, Barrack Obama, Michelle Obama, akishuka kwenye ndege hiyo na mtoto wake, Sasha.


Mke wa Rais wa Marekani, Barrack Obama 'First lady' akikumbatiana na Rais Jakaya Kikwete, mara baada ya kuwasili uwanjani hapo na mumewe (kulia), leo mchana.


 Rais Obama akipokea maua kutoka kwa mtoto Zakia Minja, uwanjani hapo.


Rais Barrack Obama akiongozana na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete mara baada ya kuwasili uwanjani hapo jana mchana.


Rais Obama akikagua gwaride lililoandaliwa kwa ajili yake mara baada ya kuwasili na kupigiwa mizinga 21.


Rais Obama akitoka kukagua gwaride lililoandaliwa kwa ajili yake mara baada ya kuwasili na kupigiwa mizinga 21, uwanjani hapo jana.


Rais Barrack Obama akiwa na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete akipokea gwaride la heshima uwanjani hapo, mara baada ya kuwasili jana mchana.


Rais Barrack Obama akisalimiana na mke wa Rais Kikwete, Mama Salama mara baada ya kupokea gwaride la heshima uwanjani hapo.


 Rais Barrack Obama, akisalimiana na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.


 Akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd.


 Hapa akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.


 Akisalimiana na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Didas Masaburi.


Hapa Rais Obama na mwenyeji wake, Rais Kikwete, wakifurahia ngoma ya Mganda ya asili ya Wangoni, mkoani Songea.


Hapa Rais Barrack Obama akiongozana na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya kuondoka Uwanja wa ndege.


Wananchi wakiwa wamekusanyika nje ya jengo la Ikulu kwa ajili ya kumkaribisha Rais Barrack Obama.


Wananchi waliokusanyika nje ya jengo la Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumkaribisha Rais Barrack Obama,wakipunga bendera za Tanzania na Marekani. 





Maofisa na baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wakiwa nje ya Ikulu, kumkaribisha Rais, Barrack Obama.


Mke wa Rais Jakaya Kikwete, Mama Salma (kulia), akiwa na mgeni wake, First lady, Michelle Obama, kwenye Ofisi za Wama.


Hapa wakiwa Makumbusho ya Taifa, wakipokea mau kwa ajili ya kuweka kwenye mabaki ya vifaa vilivyolipuliwa na bomu kwenye Ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam.


Wake hao wa Marais wa Marekani na Tanzania, wakiweka mashada hayo kwenye mabaki hayo kwa ajili ya kuwakumbuka waliopoteza maisha yao kwenye tukio hilo.


Wakiwaombea wahanga hao, mara baada ya kuweka mashada hayo ya maua.


Rais Obama Akionyesha Shoo ya Kabumbu Ubungo

Rais  Jakaya Kikwete  wa  Tanzania  akimpasia mpira  Rais  Barack Obama wa Marekani  leo kama  sehemu ya kuonyesha  uwezo  wao  kisoka pia

Hapa  Rais  Obama  akionyesha  ujuzi  katika  soka eneo la Ubungo




Rais Jakaya  Kikwete  kulia akimtazama  Rais wa Marekani Barack Obama akionyesha uwezo  wake katika  soka eneo la Ubungo  leo
Mbali ya  kuwa Rais wa dunia  pia katika  soka yumo  Rais Obama 


  Rais Obama na  Kikwete watembelea mradi wa Umeme wa Symbion Ubungo

8E9U0188 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na mwenyeji wake Rais Barrack Obama wa Marekani wakipata maelezo juu ya kituo cha uzalishaji wa Umeme Ubungo kinachoendeshwa na kampuni ya symbion power wakati viongozi hao walipofanya ziara katika kituo hicho leo asubuhi.Watatu kushoto ni Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Symbion Power Bwana Paul Hinks(picha na Freddy Maro) 8E9U9730 8E9U0198

Serikali ya Marekani imeahidi kufungua ukurasa mpya kwa Nchi za Afrika Mashariki kwa kuongeza uwekezaji katika sekta mbalimbali ili kuinua uchumi wan chi hizo.

Kauli hiyo ilitolewa jana  mjini Dar es salaam na Rais Barack Obama kwenye hotuba yake kwa wafanyabiashara wakati wa ziara yake ya siku mbili nchini Tanzania.

Alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza kiwango cha bidhaa kutoka Nchi za afrika Mashariki kuingia nchini Marekani na hivyo kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na kiuchumi kwa manufaa ya pande zote.

 “Sasa ni wakati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwekeza nchini Marekani  ili kuongeza mauzo yake nchini Marekani hadi ifike asilimia 40,” alisema Rais Obama.


Aliongeza kuwa pia ushirikiano huo unapaswa kuboresha utoaji wa mizigo katika bandari ya Dar  es salaam na Mombasa  kwenda nchi zisizo na bandari ili kuinua uchumi wa eneo hilo kwa kupunguza muda wa mizigo kukaa bandarini.

Akizungumzia hotuba ya Rais Obama Mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye viwanda nchini (CTI) Felix Mosha alipongeza hotuba hiyo kwa kufungua ukurasa mpya kwa nchi za Afrika na Marekani kwa kuonyesha kuwa wakati wa kutegemea misaada umepitwa na wakati badala yake ni kushirikiana katika uwekezaji.
Katika mkutano huo kiasi cha wafanyabiashara 170 walihudhuria mkutano huo

picha na habari kwa hisani ya Zenjinews; Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com na Francis Godwin Mzee wa matukio

No comments:

Post a Comment