Tuesday, July 23, 2013

MIILI YA WANAJESHI WA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA YAWASILI KIWANJA CHA NDEGE CHA ZANZIBAR


  Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakiwa wamebeba jeneza la Koplo Mohamed Juma Ali aliyeuawa Daafur katika harakati za kulinda amani chini ya Kikosi cha  Umoja wa Mataifa (Unamid) baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Zanzibar Jana.
  Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakiwa wamebeba jeneza la Sajent Shaibu Shehe Othman aliyeuawa Daafur katika harakati za kulinda amani chini ya Kikosi cha  Umoja wa Mataifa (Unamid) baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Zanzibar  jana.
 Baadhi ya Wanajeshi wakiwa wamebeba Majeneza ya Maiti za Marehemu Sajent Shaibu Shehe Othman na Koplo Mohamed Juma Ali waliofariki Daafur katika harakati za kulinda amani chini ya Kikosi cha  Umoja wa Mataifa, mara baada ya kuwasili kiwanja cha ndege cha Zanzibar jana .
Mke wa marehem Sajent Shaibu Shehe Othman mwenye Juba jeusi akiwa ameshikiliwa na ndugu na Askari kutokana huzuni alokuwa nayo mara baada ya kuwasili mwili wa Mume wake.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar
---
Miili ya Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ waliouawa Darfur wiki iliyopita  Sajent Shaibu Shehe Othuman wa Mpendae na Koplo Mohamed Juma Ali wa Kwarara imekabidhiwa jana kwa familia zao mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Zanzibar.

Marehemu hao wawili wenye Asili ya Zanzibar ni miongoni mwa Askari saba wa JWTZ waliuawa walipokuwa wakilinda amani chini ya Umoja wa Mataifa na Afrika UNAMID,huko Darfur. Miili ya marehemu hao imewasili majira ya saa 9 alasiri kwa ndege ya JW 90 34 aina ya Boing ikitokea katika Hospitali ya JWTZ Lugalo Jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya kuwasili Uwanjani hapo Miili ya Marehem hao ilipokelewa na Katibu mkuu Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais Khalid Mohamed Salum akifuatana na Mwenyeji wake Bregedia Jeneral Kamanda wa Bregedi ya Nyuki Sharif Sheikh Othuman Viongozi wa Vyama na Serikali,Wanafamilia pamoja na Wananchi kwa ujumla. Aidha huzuni ziliendelea kutanda kwa ndugu na Jamaa waliofika kupokea maiti hizo za 

Wapiganaji wa Amani ya Dunia chini ya mwamvuli wa UNAMID. Kwa mujibu wa Taarifa kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Shughuli za Mazishi zitafanyika kesho saa nne za asubuhi  katika makaburi ya Mwanakwerekwe nje kidogo ya Mji wa Zanzibar. Aidha shughuli hiyo ya Mazishi itaambatana na taratibu za kijeshi zitakazofanyika Makaburini hapo.
 
source: haki ngowi

No comments:

Post a Comment