Sunday, March 29, 2015

Gwajima azimia akihojiwa Polisi na kuwahishwa hospitalini



ASKOFU wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima JANA alizimia na kisha kukimbizwa hospitali wakati akihojiwa Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.
Gwajima ambaye alijisalimisha kituoni hapo saa 8:22 jana mchana akiitikia wito wa polisi uliomtaka kufika kutokana na tuhuma za kutoa lugha chafu dhidi ya Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki JIMBO Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Waandishi wa Mtanzania Jumamosi waliokuwa kituoni hapo wanaeleza kuwa walimuona Gwajima akitolewa kutoka katika chumba cha mahojiano akiwa amebebwa.

Kwa mujibu wa waandishi hao Gwajima ambaye alikuwa amebebwa na maofisa wa polisi alipelekwa moja kwa moja kwenye GARI aina ya Noah kwa ajili ya kumpeleka hospitali.

Tukio hilo lililotokea majira ya saa 3:16 usiku lilikuja katika kipindi kisichozidi dakika saba tangu askofu huyo alipoonekana akiwa ameshikiliwa na wasaidizi wake kuelekea msalani huku yeye mwenyewe akiwa amejishika kichwa.

Wakati akipelekwa hospitali, msafara wake ulikuwa ni wa magari mawili mojawapo likiwa ni aina ya TOYOTA LAND CRUISER lenye namba za usajili PT 1848 na Noah yenye namba za usajili T 215 BEM.
Akizungumza na gazeti hili kituoni hapo, mwanasheria wa askofu huyo, JOHN Mallya alisema wakati wakiwa katika mahojiano, alisema anahisi kizunguzungu na baadaye akaishiwa nguvu na akawa amefumba macho.

Mallya alisema baada ya hali hiyo kutokea, polisi walimchukua na kisha kumpeleka katika hospitali ya Jeshi la Polisi iliyoko Kurasini, Dar es Salaam.

Wakati Mallya akiwasiliana na gazeti hili majira ya 4:30 usiku alisema kuwa walikuwa wakifanya mchakato wa kumuhamishia katika hospitali ya TMJ kutokana na yake kutokuwa nzuri.

“Siwezi kujua tatizo ni nini na siwezi kuzungumza chochote kuhusu hilo maana hayo ni mambo ya kitabibu” alisema Malya.

Ilipotimu saa 4:41 Waandishi wa gazeti hili ambao nao walifika katika hospitali hiyo ya Jeshi la Polisi walishuhudia Gwajima akitolewa katika hospitali hiyo ya Jeshi la Polisi na kisha kupakizwa katika GARI maalum la kubebea wagonjwa lenye namba DFP 6309.

Wakati hayo yakitokea taarifa nyingine zilizolifikia gazeti hili zilidai kuwa; kwa muda wote akiwa katika mahojiano, Gwajima alikuwa hajala chochote hali ambayo iliibua wasiwasi kwamba huenda ilichangia kubadilika kwa afya yake.

Polisi mmoja aliyekuwa katika chumba cha mahojiano aliwaeleza waandishi wetu kwamba Askofu Gwajima alipoteza fahamu muda mfupi baada ya kuhojiwa kuhusu mali anazozimiliki.

Awali wakati Gwajima alipowasili kituoni hapo mchana kabla ya kuhojiwa alizungumza na waandishi wa habari ambapo alikiri kutoa lugha chafu dhidi Kardinali Pengo.

Gwajima ambaye alifika kituoni hapo saa 8:22 mchana alisema kauli yake hiyo ambayo imesambaa kwenye mitandao ya kijamii aliitoa kutokana na Kardinali Pengo kuwageuka wenzake ambao ni Baraza la Maaskofu Tanzania linalounganisha Wakatoliki, Pentekoste na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kukubaliana kwa pamoja kuwa hawataki Mahakama ya Kadhi.

Alisema maaskofu wote walikubaliana kuhusu tamko hilo na kisha kulisaini lakini anamshangaa Kardinali Pengo ambaye pia alisaini kuwageuka.

“Mimi KAMA kiongozi wa kiroho nikaona nimkemee kiongozi mwenzangu wa kiroho aache mambo ambayo si mazuri. Hakuna maneno ya kashfa ambayo nimeyatoa. Niliyotoa ni neno la Mungu linalotumiwa kumwongoza mtumishi wa Mungu,” alisema Gwajima.

Alisema anashangaa kuitwa polisi kwani hajatukana polisi na ndio sababu akaitika wito na kufika.

Gwajima alifika polisi akitembea kwa miguu kutokana na foleni kali iliyokuwepo barabarani huku akiwa ameongozana na Mwanasheria wake JOHN Malya pamoja na baadhi ya wachungaji, waumini wa kanisa hilo na wengine waliotajwa kuwa ni walinzi wake.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Kamishna Suleimani Kova alisema Mchungaji Gwajima ametii amri ya Jeshi hilo KAMA alivyotakiwa.

Kova alisema baada ya kufika kituoni hapo alielekezwa kwenda kumuona Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam SACP Costantine Massawe.

Akitaja tuhuma zinazomkabili Mchungaji Gwajima, Kova alisema ni pamoja na kumkashifu na kumtukana hadharani kiongozi wa Kanisa Katoliki Kardinali Pengo.

“Taratibu za kuhojiwa zimeshaanza kwa mujibu wa sheria na mtuhumiwa atapewa haki zote anazostahili ikiwemo kuwa na ndugu yake wa karibu, rafiki anayemwamini au wakili wake. KAMA ilivyokawaida utakusanywa ushahidi kutoka pande zote za shauri hilo ili kubaini ukweli wa jinsi tukio hilo lilivyotokea,” alisema Kova.

Kova alisema baada ya hapo hatua nyingine za kisheria zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kupata maoni ya kitaalamu na ya kisheria ili kuhakikisha kwamba haki inatendeka.

“Ili ufanisi upatikane katika upelelezi wa shauri hili ni muhimu kupata ushirikiano kutoka kwa kila atakayetakiwa kulisaidia Jeshi la Polisi kukamilisha haraka upelelezi wa shauri hilo ambalo limepata mvuto mkubwa kwenye jamii,” alisema Kova.

Katika video na sauti zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii hasa What’s APP, Gwajima alirekodiwa akiwa kwenye ibada ya kanisa lake akitumia lugha zisizokuwa na staa kwa Kardinali Pengo akimtuhumu kuwa ni msaliti kwani amekwenda kinyume na Taasisi ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Baraza la Makanisa ya Kipentekoste (CPCT) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kwa kuwataka waumini waisome Katiba Inayopendekezwa kisha wapewe uhuru wa kupiga kura ya “ndiyo” au “hapana” tofauti na vyombo hivyo vyenye dhamana ya kuongoza dini ya Kikristo vilivyotaka waumini waipigie kura ya “hapana”.

  • Asifiwe George na Humphrey Shao via gazeti la MTANZANIA
  • Picha zimepatikana via WhatsApp
  • SOURCE: WAVUTI
  • Sunday, March 22, 2015

    ZITTO RASMI ACT, APEWA KADI NAMBA 007194, KUONGEA NA WANAHABARI LEO

    Zitto Kabwe akikabidhiwa rasmi kadi ya uanachama wa ACT.
    HAYAWI hayawi…Sasa yamekuwa licha ya kusemwa sana kwa muda mrefu juu ya kuhusishwa na chama kipya cha siasa cha ACT-Tanzania dhidi ya aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Ruyagwa Kabwe sasa yamekuwa kweli kwa Mbunge huyo baada ya jana Jumamosi ya Machi 21, kupokelewa rasmi na chama hicho na kukabidhiwa kadi yake yenye namba 007194.

    Zitto akionyesha kadi yake kwa wanachama wa ACT.
    Hii inafuatia siku moja baada ya Zitto kutangaza kuachia…
    Zitto Kabwe akikabidhiwa rasmi kadi ya uanachama wa ACT.
    HAYAWI hayawi…Sasa yamekuwa licha ya kusemwa sana kwa muda mrefu juu ya kuhusishwa na chama kipya cha siasa cha ACT-Tanzania dhidi ya aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Ruyagwa Kabwe sasa yamekuwa kweli kwa Mbunge huyo baada ya jana Jumamosi ya Machi 21, kupokelewa rasmi na chama hicho na kukabidhiwa kadi yake yenye namba 007194.
    Zitto akionyesha kadi yake kwa wanachama wa ACT.
    Hii inafuatia siku moja baada ya Zitto kutangaza kuachia ubunge na kuandika barua rasmi ambapo sasa amekuwa mwanachama wa ACT-Tanzania na kuahidi kuendeleza mapambano ndani ya chama hicho.
    Kadi ya Zitto Kabwe yenye namba 007194.
    Hata hivyo, kwa mujibu wa viongozi waandamizi wa ACT-Tanzania wamedokeza kuwa, Zitto ataongea na vyombo vya habari leo Jumapili ya Machi 22.
    Zitto Kabwe akivalishwa skafu ya ACT mara baada ya kupokea rasmi kadi ya chama hicho jana.

    ACT-Tanzania: kirefu chake ni : Chama cha Alliance for Change and Transparence (ACT-Tanzania). Makao makuu ya chama hicho yapo Kijitonyama Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
    CREDIT: Modewji Blog

    Saturday, March 21, 2015

    BREAKING NEWZZZZZ: ZITTO KABWE AJIUZULU RASMI UBUNGE WA KIGOMA KASKAZINI USIKU HUU BUNGENI DODOMA

    Aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa Tiketi ya Chadema, Kabwe Zitto akisoma barua aliyomwandikia Spika wa Bunge, Anne Makinda kumtaarifu kuwa anang'atuka nafasi ya Ubunge. Pia aliwaaga Wabunge wenzake na kuahidi kurudi tena Mungu akijalia baada ya Uchaguzi wa mwaka huu.
    Wabunge mbalimbali wakiwepo wa Chadema, Cuf, NCCR na CCM walionekana dhahiri kububujikwa na machozi kufuatia kujivua kwake Ubunge.

    HII NDIO BARUA ALIYOISOMA BUNGENI 
    Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mhe Zitto Zuberi Kabwe usiku huu ametangaza rasmi Bungeni Dodoma kuachia kiti hicho alichokipata kupitia CHADEMA.
    Mhe. Kabwe ametangaza kung'atuka nafasi hiyo baada ya Mwenyekiti wa Bunge Mhe Mussa Hassan Zungu Kumruhusu kutoa kauli binafsi mara baada ya wabunge kumaliza kupitia vifungu vya sheria 
    ya Maafa ambayo hata hivyo haikupitishwa kwa kutotimia akidi ya wabunge ambao nusu yao hawakuwepo ukumbini.
    Mhe Zungu alimtakia kila la heri Mbunge huyo machachari ambaye amesema ameamua kuachia ngazi baada ya chama chake kumfukuza. Hata hivyo alimalizia kwa kusema kwamba anategemea kuwa nao tena mwezi Novemba mwaka huu.CHANZO :  MTAA KWA MTAA BLOG

    Monday, March 16, 2015

    YANGA SC YAWATANDIKA WAZIMBABWE 5-1

    s Huu ndio Mpira uliotumika katika Mchezo wa leo baina ya Yanga na FC Platinum katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo.
     Kikosi cha Yanga.
     Kikosi cha FC Platinum.CHANZO MTAA KWA MTAA BLOG
     Beki wa Yanga,Kelvin Yondani akiondosha hatari lakoni kwake wakati wa mchezo wa Mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika,uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
    Mshambuliaji Machachari wa Timu ya Yanga,Mrisho Khalfan Ngassa akiichambua ngome ngombe ya Timu ya Fc Platinum ya nchini Zimbabwe katika mchezo wa Mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika,uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.Yanya imeshinda Bao 5 - 1.
    Mchezaji wa Yanga,Simon Msuva akiangalia namna ya kuwatoka mabeki wa Timu ya Fc Platinum ya nchini Zimbabwe katika mchezo wa Mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika,uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.Yanya imeshinda Bao 5 - 1.
     Mrisho Ngassa akifanya yake uwanjani hapo.
    Amis Tanbwe wa Yanga na Gift Bello wa FC Platinum wakiwania mpira wa juu wakati wa mchezo wa Mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika,uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
    Salum Telela wa Yanga akiipachikia timu yake bao la kuongoza wakati wa mchezo wa Mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika,uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

     Wachezaji wa Timu ya Yanga wakishangilia ushindi wao.
     Beki wa timu ya Yanga,Juma Abdul akiangalia nafasi ya kupeleka mpira.
     Simon Msuva akichuana na Gift Bello wa FC Platinum wakati wa mchezo wa Mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika,uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
     Msuvaaa
     Furaha ya Ushindi: Kiungo mchezeshaji wa timu ya Yanga,Haroun Niyonzima akiongoza mashabiki wa Timu ya Yanga kushangia goli lao dhidi ya Fc Platinum ya nchini Zimbabwe katika mchezo wa Mashindano ya Kombe la shirikisho,uliochezwa leo kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo. Yanya imeshinda Bao 5 - 1.







    source:vijana na matukio