Sunday, March 15, 2015

ANGALIA JINSI ZITTO ALIVYOITEKA KIGOMA,MAPOKEZI YAKE YASHTUA WENGI

Mh zitto kabwe baada ya chama chake cha CHADEMA kutangaza kumfukuza uanachama ndani ya chama hicho ameamua kufanya ziara ya siku tatu ndani ya kigoma kuzumgumza na wananchi wake juu ya hali ya kisiasa inayomkabili kwa sasa,hizi hapa ni baadhi picha za mapokezi yake kigoma 

Ikiwa bado sakata la kufukuzwa uanachama kwa mbunge wa kigoma kaskazini (CHADEMA) mh ZITTO KABWE linaendelea kuchukua nafasi katika vichwa vya watanzania na wapenda siasa,mbunge huyo ameanza kufanya ziara ya siku tatu jimboni kwake kuzungumza na watanzania mbalimbali.
Akiwa katika ziara yake MBUNGE wa Kigoma Kaskazini,Zitto Kabwe(Chadema),amewataka wakazi wa mkoa wa kigoma wasisikitishwe na mambo yanayomkabili kwa sasa kwa kile alichoeleza kuwa asilimia kubwa ya wanasiasa makini walishapitia misuko suko kama yake.
Amewaeleza kuwa jambo la msingi ni kumuunga mkono katika hatua yoyote atakayochukua kwa ajili ya wanakigoma na Taifa kwa ujumla katika kumaliza mgogoro uliopo baina ya Chama chake na yeyeZitto ametoa kauli hiyo leo mjini Kigoma alipokutana na viongozi 250 kwenye mkutano wa ndani uliohusisha viongozi kutoka katika kila kijiji kwenye jimbo la Kigoma kaskazini yenye jumla ya vijiji 45.Aliwataja baadhi ya wanasiasa waliopita katika hatua kama yake na baadae wakageuka washindi kuwa ni Maalim Seif Sharif Hamad(Tanzania),Mahathir Mohamed(Malaysia na Indira Gandhi wa India.“Msinililie mimi kwa kuwa haya ni mapito ya kila mwanasiasa Makini,wengi walio makini walitofautiana na vyama vyao kwa sababu ya maslahi ya mataifa yao,wapo walioanzisha vyama baada ya hali hiyo na wakashinda na wapo waliopigiwa magoti na vyama vyao baada ya kugundua walichofanya si sahihi, hivyo jukumu kubwa ni kuniunga Mkono”alisema Zitto.
Alisema mpaka sasa hajapewa taarifa yoyote ya kusitishwa kwa Ubunge wake na kama hali hiyo ikijitokeza atarudi kuwafahamisha juu ya hatua atakayochukua
Zitto yupo mjini Kigoma kwa ziara ya siku tatu,ambapo atawatembelea wakulima wa mradi wa Kahawa walio katika mfuko wa hifadhi ya Jamii(NSSF), pamoja na kukabidhi gari aina ya Ambulance katika kituo cha Afya Nyarubanda na kisha kufanya mikutano miwili ya hadhara.
Juzi Mwanasheria mkuu wa Chadema Tundu Lissu,alitangaza hadharani kuvuliwa uanachama kwa Zitto kutokana na kushindwa katika kesi aliyofungua kupinga asijadiliwe na Chama Chake

                                   source:matukio na vijana

No comments:

Post a Comment