Monday, March 9, 2015

KOCHA WA YANGA AGOMA KUMPA MKONO KOCHA MWENZIE

Kocha simba akimpa mkono kocha wa Yanga
Hans ameshindwa kupeana mkono wa pongezi na kocha mwenzake kutokana na kikosi chake kukubali kupokea kichapo kutoka kwa wekundu wa msimbazi lakini katika hali ya kawaida mchezo ukimalizika makocha upeana mkono kama ishara ya kukubali matokeo (fair play) na kocha msaidizi wa yanga Boniface Mkwasa ametoa mkono huku akiwa ameangalia pembeni.
Goran akimwambia basi samahani kwa kukufunga wewe nipe mkono tu
Baada ya mchezo kocha aliwashukuru wachezaji wake kwa kuonesha mchezo mzuri huku zaidi akiwapongeza mashabiki waliofurika kwenye uwanja wa taifa kwa kuwaunga mkono.
Boniface Mkwasa akitoa mkono kwa mashaka mara baada ya mkuu wake kushindwa kutoa kabisa
Kwa matokeo hayo simba imefikisha pointi 26 na imekalia nafasi ya tatu.

source: matukio na vijana

No comments:

Post a Comment