Monday, March 16, 2015

ZITTO KABWE ATANGAZA RASMI KUTOGOMBEA UBUNGE HUKO KIGOMA 2015,VILIO VYATAWALA JIMBONI

Wakazi wa Kigoma Kaskazini leo walikusanyika pamoja kumsikiliza Mbunge wao Zitto Kabwe ambaye siku ya leo ameamua kuitumia rasmi kama kuwaaga wananchi na wapiga kura wa jimbo lake.
Zitto Kabwe ambaye Ijumaa ya wiki hii kupitia mtandao wa kijamii kwenye akaunti yake ya Twitter ali break news kwamba hatogombea tena Ubunge kwenye uchaguzi ujao wa mwishoni mwa mwaka huu.
Baada ya hotuba yake kumalizika,Mtandao huu ulifanikiwa kuongea na baadhi ya wananchi lakini asilimia kubwa ya wananchi hawajamuunga mkono kwa uamuzi huo wa Mbunge wao Zitto Kabwe wa kutogombea tena ubunge na wengine walikwenda mbali zaidi na kusema kuwa kazi bado haijaisha, pia katika hotuba yake hiyo alisema kuwa ndani ya wiki inayoanza kesho watu watarajie makubwa na wala wasishtuke kutokana na uamuzi atao uchukua. 
Kwa tetesi zilizo chini ya kapeti hapa mjini Zitto Kabwe anataka kuja kugombea jimbo la kigoma mjini, hizi ni baadhi ya picha mtu wangu.


 
Bonyeza {HAPA kusoma Hotuba yake aliyoitoa leo jimboni kwake kwa kirefu zaidi

source: vijana na matukio

No comments:

Post a Comment