Saturday, May 4, 2013

Kauli za Bungeni zilizowaacha Wananchi na vijiulizo

"Kaa chini, mbona unawashwawashwa... Kaa chini. Usitafute umaarufu hapa..." Mwenyekiti wa Bunge, Sylvester Mabumba (CCM) akimnyamazisha John Mnyika, Mbunge wa Ubungo (CHADEMA).

"Kwa kuwa wanaume wengi wanabaka, kifunguliwe kituo wafundishwe kutongoza.” Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA), Leticia Nyerere.

‘‘Kuna wabunge ambao wana mimba sizizotarajiwa Bungeni...” Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde.

“Sikufurahishwa na kauli ya Lusinde kwamba tuna mimba sizizotarajiwa.”  Anna Abdallah (Viti Maalum, (CCM).

“UDOM (Chuo Kikuu cha Dodoma) kuna udini wa hali ya juu, wanafunzi wa dini tofauti hawalali chumba kimoja.”
Mbunge wa Rombo (CHADEMA), Joseph Selasini.

“Serikali ina tatizo kwa kuwa kuna akili ndogo inatawala vichwa vikubwa.” Mbunge wa Iringa Mjini (CHADEMA), Mchungaji Peter Msigwa.

‘‘Siongei na mbwa bali naongea na mwenye mbwa.” Mbunge wa Kondoa Kusini (CCM), Juma Nkamia

‘‘Mambo mengi nchi hii hayaendi kutokana na serikali pumbavu, hatuwezi kuwa na waziri wa elimu boya...”
Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA, Joseph Mbilinyi.

“Serikali iruhusu raia wa Tanzania walime bangi wapate fedha za kigeni.” Mbunge wa Nkasi (CCM), Ally Keissy.

No comments:

Post a Comment